• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Industry,Trade and Investments
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Human Resources Management and administration
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Communit Development
    • Vitengo
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
      • Procument Management
      • Government Communication
      • Finance and Accounts
      • Sports, Culture and Arts
      • Waste Management and Sanitation
      • Natural Resources and Environment Conservation
    • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Other Laws
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
      • iCHF
      • Lishe
      • Social welfare
    • Elimu
      • Pre and Primary Education
      • Elimu Sekondari
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
      • Ten Percent Loans
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

DC KHERI ARIDHISHWA NA MIKAKATI YA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA SHULE

Posted on: June 23rd, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Kheri Denice James ameridhishwa na mikakati iliyowekwa na Manispaa ya U bungo ya kuboresha miundombinu ya shule ikwemo utengenezaji wa madawati na ujenzi wa madarasa katika shule za manispaa hiyo ikiwa ni maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wa darasa la kwanza na kitado cha kwanza kwa mwaka 2022.

Mhe. Kheri ametoa kauli hiyo leo juni 23, 2021 wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika manispaa hiyo na kueleza kuwa mkakati wa kujenga madarasa na kutengeneza madawati mapema utaondoa changamoto ya upungufu wa miundombinu hiyo kwenye shule na hivyo kufanya wanafunzi kusoma katika mazingira bora.

“Kwa mwaka 2022 sitegemei Ubungo iwe kati ya Halmashauri zenye changamoto ya upungufu wa madarasa na madawati ikiwa mikakati yetu itatekelezwa kwa ufanisi na hii itafanikwa zaidi jamii na wadau wa maendeleo wakishirikishwa kikamilifu katika kulitekeleza hili, kila mmoja atekeleze wajibu wake” alieleza Mhe. Kheri

Mhe. Kheri ameendelea kusema kuwa, kama  idadi ya wanafunzi wanaoratajia kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka ujao tunayo ni dhahiri mahitaji ya madarasa na madawati yatakayotumika yanajulikana hivyo  naagiza madarasa hayo  yaanze kujengwa mapema  mwezi  julai  na hadi mwezi disemba yawe yamekamilika tayari kwa kuwapokea wanafunzi januari 2022.

Aidha, Mhe. Kheri amewapongeza wadau wa maendeleo wakiwemo benki ya CRDB, NMB na Kanisa Katoliki  kwa mchango wao mkubwa katika kuboresha miundombinu ya shule ya sekondari mashujaa iliyoko kata ya Sinza  kwa kujenga madarasa, fensi na  utengenezaji wa viti na meza hali inayoifanya shule hiyo kuwa na mazingira mazuri ya kujifunza na kujifunzia

“Huu mkakati wa kuboresha miundombinu katika shule zetu unapaswa kuwa shirikishi ili kila mtu awe na mchango katika kufanikisha zoezi hili mfano mzuri ni katika shule ya sekondari mashujaa ambapo kanisa katoliki limetoa milioni 20 kwa ajili ya ujenzi wa ukuta wa shule, nawashukuru na kuwapongeza sana viongozi wengine tuige mfano wa uongozi wa shule hiinamna ulivyoshirikisha wadau”

Mhe. Kheri amezitaka bodi na kamati za shule zote za Manispaa ya Ubungo kutekeleza majukumu yao ipasavyo katika kusimamia na kubuni mikakati itakayozifanya shule zetu kuondokana na changamoto mbalimbali ikiwemo madarasa na madawati  badala ya kusubiri serikali pekee itatue changamoto hizo.

“ifike wakati bodi na kamti za shule zishindanishwe kwa ubunifu wa kuboresha miundombinu ya shule hii itasaidia kuwakumbusha wajumbe majukumu yao ya msingi badala ya kufanya kazi kwa mazoea” alielekeza Mhe. Kheri.

Akieleza moja ya  mkakati wa manispaa, Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Beatrice Dominic amesema kuwa pamoja na ujenzi wa madarasa unaoendelea katika shule mbalimbali, kwa mwaka  mpya wa fedha unaonza mwezi Julai 2021 manispaa imepanga kujenga madarasa 100 lengo likiwa ni kuhakikisha changamoto ya upungufu wa  madarasa na madawati inapungua kwa kiasi kikubwa.

Mhe.  Mkuu wa Wilaya Ubungo  ametembelea miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 59.8 ikiwemo mradi wa ujenzi wa  kituo kikuu cha mabasi  cha magufuli kilichogharimu bilioni 56.

Taarifa

  • KIBALI CHA KUANZA KUTOZA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA MIZIGO July 17, 2023
  • KUKANUSHA TAARIFA YA UWEPO WA HARAFU MBAYA STENDI YA MABASI MAGUFULI July 06, 2023
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 Ubungo September 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KATA YA UBUNGO YAKABIDHI MKOPO WA TSH. 122,800,000/= KWA VIKUNDI SITA VYA ASILIMIA 10

    May 02, 2025
  • KAMPENI YA KATAA UCHAFU, SAFISHA, PENDESHA UBUNGO YAZINDULIWA, MITAA SAFI NA MICHAFU KUPEWA ZAWADI

    May 03, 2025
  • FANYENI KAZI, MSIJALI MASILAHI BINAFSI" ~ CHALAMILA

    May 01, 2025
  • HUDUMA YA KUJIFUNGUA KWA UPASUAJI YAANZA RASMI KITUO CHA AFYA GOBA,WANANCHI WAKARIBISHWA

    April 30, 2025
  • Tazama zote

Video

KIWANJA CHAKO KINA HATI? | UMEKUWA UKISUMBULIWA NA MIGOGORO YA ARDHI? | KARIBU KWENYE ARDHI CLINIC
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa