• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Industry,Trade and Investments
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Human Resources Management and administration
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Communit Development
    • Vitengo
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
      • Procument Management
      • Government Communication
      • Finance and Accounts
      • Sports, Culture and Arts
      • Waste Management and Sanitation
      • Natural Resources and Environment Conservation
    • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Other Laws
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
      • iCHF
      • Lishe
      • Social welfare
    • Elimu
      • Pre and Primary Education
      • Elimu Sekondari
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
      • Ten Percent Loans
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

DC UBUNGO AWATAKA DAWASA KUFUATA RATIBA ZA MGAO WA MAJI UBUNGO

Posted on: November 10th, 2022


- Leo Novemba 10, 2022 Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Kheri James amefanya kikao kazi kati ya wenyeviti wa serikali za mitaa na Mameneja wa DAWASA Wilaya ya Ubungo ili kufanya tathmini ya changamoto ya maji iliyopo sasa pamoja na kuweka mikakati ya kumaliza changamoto hiyo kwa Wilaya ya Ubungo

- Katika kikao hicho James amesema kuhusu tatizo la maji linaloikumba Dar es Salaam kwa sasa ni lazima kwanza kukubali kuwa tatizo lipo kisha kuendelea kutekeleza mikakati ya kumaliza tatizo hilo ambalo limesababishwa na kupungua kwa kina cha maji katika mto Ruvu.

- Kwasasa serikali imekuja na mpango wa kuchimba na kufufua visima vya maji ambavyo vitaongeza maji kwenye mfumo mzima wa DAWASA na kupelekea ahueni kwa wananchi

- Wakiongea katika kikao hicho baadhi ya wenyeviti wa Serikali za mitaa wamesema kuwa DAWASA ihakikishe inatekeleza ratiba ya mgao walioweka na kama kutakua na mabadiliko ya ratiba hiyo kuwe na taarifa mapema ili wananchi waelewe

- Aidha kwa upande mwingine James amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa mikakati aliyoelekeza kukabiliana na tatizo hili la maji ikiwemo mpango wa kufufua visima kale na kuchimba visima vipya ambapo siku ya kesho Rais Samia anatarajiwa kukabidhi mitambo kwaajili ya kuchimba visima hivyo katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Ubungo na Dar es Salaam kwa ujumla
"Mhe. Rais anafanya kazi kubwa sana kukabiliana na tatizo la maji kwa Dar es salaam nzima. Wenyeviti muwe wa kwanza kutambua na kumtia moyo Mhe. Rais kwa kazi nzuri na kubwa anayoifanya" Alisema

- Wakati kikao hicho kikiendelea, Mhe. Mkuu wa wilaya alifanya mawasiliano kwa njia ya simu na Waziri wa Maji Mhe. Juma Aweso ambapo amewaondoa hofu wenyeviti hao kuhusu tatizo la maji ambalo juhudi zinaendelea kufanyika kupunguza adha hiyo. Aweso pia amewapongeza mameneja wa DAWASA kwa wilaya ya Ubungo kwa kazi kubwa wanayoendelea kuifanya kukabiliana na changamoto hii.

- Akijibu hoja za Wenyeviti Meneja wa DAWASA Kibamba ndugu Elizabeth Sankere amesema kuwa hoja zote wamezichukua na wameahidi kuzifanyia kazi haraka sana kutoka sasa. Kwa upande mwingine Sankere amewapongeza wenyeviti hao kwa kutoa ushirikiano kwa DAWASA

@dawasatz

#ubungoyetufahariyetu
#dawasa

Taarifa

  • KIBALI CHA KUANZA KUTOZA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA MIZIGO July 17, 2023
  • KUKANUSHA TAARIFA YA UWEPO WA HARAFU MBAYA STENDI YA MABASI MAGUFULI July 06, 2023
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 Ubungo September 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KATA YA UBUNGO YAKABIDHI MKOPO WA TSH. 122,800,000/= KWA VIKUNDI SITA VYA ASILIMIA 10

    May 02, 2025
  • KAMPENI YA KATAA UCHAFU, SAFISHA, PENDESHA UBUNGO YAZINDULIWA, MITAA SAFI NA MICHAFU KUPEWA ZAWADI

    May 03, 2025
  • FANYENI KAZI, MSIJALI MASILAHI BINAFSI" ~ CHALAMILA

    May 01, 2025
  • HUDUMA YA KUJIFUNGUA KWA UPASUAJI YAANZA RASMI KITUO CHA AFYA GOBA,WANANCHI WAKARIBISHWA

    April 30, 2025
  • Tazama zote

Video

KIWANJA CHAKO KINA HATI? | UMEKUWA UKISUMBULIWA NA MIGOGORO YA ARDHI? | KARIBU KWENYE ARDHI CLINIC
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa