• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Industry,Trade and Investments
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Human Resources Management and administration
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Communit Development
    • Vitengo
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
      • Procument Management
      • Government Communication
      • Finance and Accounts
      • Sports, Culture and Arts
      • Waste Management and Sanitation
      • Natural Resources and Environment Conservation
    • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Other Laws
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
      • iCHF
      • Lishe
      • Social welfare
    • Elimu
      • Pre and Primary Education
      • Elimu Sekondari
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
      • Ten Percent Loans
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

DIWANI KIMWANGA AWATOA HOFU WAZAZI KUHUSU UTEKAJI WA WATOTO

Posted on: July 24th, 2024

Diwani wa Kata ya Makurumla Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo mkoani Dar es Salaam, Bakari Kimwanga, amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanakuwa na utulivu hasa kutokana na taharuki ya utekaji watoto kwenye shule.

Pamoja na hali hiyo amesema kuwa mpaka sasa ndani ya Kata ya Makurumla hakuna tukio la kutekwa kwa mtoto huku akiweka wazi ni lazima kila mwana jamii ahakikishe anatoa ulinzi kwa mtoto hasa wanapokuwa mitaani.

Kauli hiyo ametoa Julai 23, 2024 alipokuwa akizungumza na wazazi, walezi na walimu katika shule za Msingi za Mianzini,  Karume na Dk. Omari, ambapo juzi ilizuka taharuki ya kutekwa watoto kwenye shule hizo na kuibua Sintofamu kwa wazazi kulazimika kuvamia shule ili kuona usalama wa watoto wao.

"Tangu zilipoibuka taarifa hizi za taharuki Julai 22, 2024 (Jumatatu), tumefuatilia taarifa kwenye shule zetu, vyombo vya ulinzi na usalama kwa maana ya Jeshi la Polisi hali iko shwari wazazi wenzangu.

"Wale waliopata taharuki na kuja shule hawajakosea kwa sababu wamefanya hivyo kwa lengo la kutaka kujua usalama wa watoto. Najua mama zetu uchungu mkubwa wanaoupata hasa kuhusu watoto. Wazazi wenzangu naomba tuwe na tulivu hali iko shwari kubwa tusisahau wajibu wetu wa malezi na usalama kwa watoto hata wanapokuwa nyumbani," amesema Diwani Kimwanga

Aidha, amewataka wazazi kutambua kuwa ni lazima wanaweka mkazo kwenye suala la lishe kwa watoto kwa kuhakikisha wanachangia Shilingi 500 ya chakula kama walivyokubaliana kwenye mikutano ya wazazi jambo ambalo litamsaidia mtoto kupata chakula shuleni badala ya kwenda mitaani wakati wa kipindi cha mapumziko

Kwa upande wake Afisa Elimu Msingi, Manispaa ya Ubungo, Denis Nyoni amewataka wazazi kuwa na utulivu kwani hadi kufikia jana hakuna taarifa za watoto kutekwa katika shule kwenye manispaa hiyo.

"Naomba walimu msisahau wajibu wa kuandika mahudhurio ya watoto kila siku wawapo darasani na hata wakati wanapomaliza masomo kwa siku majina yaitwe. Hatua hii ndio njia ya kuendelea kudhibiti usalama wa watoto wetu," amesema Nyoni

Taarifa

  • KIBALI CHA KUANZA KUTOZA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA MIZIGO July 17, 2023
  • KUKANUSHA TAARIFA YA UWEPO WA HARAFU MBAYA STENDI YA MABASI MAGUFULI July 06, 2023
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 Ubungo September 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KATA YA UBUNGO YAKABIDHI MKOPO WA TSH. 122,800,000/= KWA VIKUNDI SITA VYA ASILIMIA 10

    May 02, 2025
  • KAMPENI YA KATAA UCHAFU, SAFISHA, PENDESHA UBUNGO YAZINDULIWA, MITAA SAFI NA MICHAFU KUPEWA ZAWADI

    May 03, 2025
  • FANYENI KAZI, MSIJALI MASILAHI BINAFSI" ~ CHALAMILA

    May 01, 2025
  • HUDUMA YA KUJIFUNGUA KWA UPASUAJI YAANZA RASMI KITUO CHA AFYA GOBA,WANANCHI WAKARIBISHWA

    April 30, 2025
  • Tazama zote

Video

KIWANJA CHAKO KINA HATI? | UMEKUWA UKISUMBULIWA NA MIGOGORO YA ARDHI? | KARIBU KWENYE ARDHI CLINIC
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa