• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Industry,Trade and Investments
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Human Resources Management and administration
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Communit Development
    • Vitengo
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
      • Procument Management
      • Government Communication
      • Finance and Accounts
      • Sports, Culture and Arts
      • Waste Management and Sanitation
      • Natural Resources and Environment Conservation
    • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Other Laws
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
      • iCHF
      • Lishe
      • Social welfare
    • Elimu
      • Pre and Primary Education
      • Elimu Sekondari
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
      • Ten Percent Loans
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

MANISPAA YA UBUNGO YATOA BILIONI 1.1 KWA VIKUNDI 111

Posted on: January 7th, 2021

Manispaa ya Ubungo jijini Dar Es salaam leo januari 7 2020 imetoa mikopo isiyo na riba yenye thamani ya shilingi bilioni 1.1 kwa vikundi  111 vya  wanawake, vijana na watu wenye ulemavu  kwa ajili kuendeleza na kukuza mitaji  ya biashara zao na hatimaye kujikwamua na umasikini.

Mikopo hiyo iliyotolewa leo baada ya kupata mafunzo ya namna ya kuendesha biashara zao kwa vikundi hivyo vyenye wanufaika  1566 ambapo vikundi vya wanawake 62 vitapata shilingi milioni 560,135,200, milioni 424 161,000 kwa vikundi 38  vya vijana na  milioni 119 , 000, 000 kwa ajili ya vikundi 11 vya watu wenye ulemavu.

Wanufaika wa mikopo wakifuatilia mafunzo kabla ya kukabidhiwa mikopo


Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo na kutoa hundi ya mikopo kwa vikundi hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Kisare Makori  amewaeleza wajasiliamali hao kuwa utoaji wa mikopo hiyo ni utekelezaji wa sera ya serikali inayozitaka Halmashauri kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya kuwezesha wananchi kiuchumi na kuondokana na umasikini

Makori amesema kuwa "Nawapongeza kwa kukidhi vigezo na kupata mikopo hii, nawasii  mkaitumie mikopo hii kwa ajili ya kukuza biashara zenu na sio kununua vijora vya sherehe kwani serikali imeamuankutoa mikopo hii isiyo na riba ili ujasiriamali uwe njia ya kumkwamua mwananchi kiuchumi kwa kukuza mitaji yao"

Makori ameendelea kueleza kuwa utoaji wa mikopo hiyo unaenda  sambamba na kufanya marejesho kwa wakati ili kuongeza fursa kwa watu wengine kupata mikopo lakini pia kuongeza kiwango cha kukopesha " hivyo rejesheni mikopo kwa wakati"

"Tusififishe ndoto na nia njema ya serikali ya kukuza uchumi wa wananchi kwa kutorejesha, hengeni nidhamu na uaminifu kwenye marejesho ili tupanue wigo wa kukopesha watu wengi zaidi na kutengeneza mabilioni" amesisitiza Makori

Kwa upande wake mratibu wa mfuko wa wanawake vijana na walemavu wa manispaa hiyo Elizabeth Kebwe ameeleza kuwa vikundi vinavyopata mkopo awamu hii vinajishughulisha na shughuli za kilimo,  mifugo, uzalishaji mali, usindikaji wa bidhaa mbalimbali, viwanda vidogovidogo ambavyo vimekidhi vigezo wa kupata mkopo.

Kebwe amesema kuwa kwa  kipindi cha miaka 3 kuanzia mwaka 2017 hadi 2019, Manispaa imefanikiwa kutoa mikopo yenye thamani ya shilingi 3,966,405,785 kwa vikundi 914 yenye wanufaika 9281 na kati ya fedha hizo shilingi 1,031,003, 687.25 ndio zimerejeshwa.


Aidha Elizabeth kebwe amefafanua kuwa mikopo inayotolewa leo kuna  vikundi vitapata mkopo wa milioni 70 kikiwa ndicho kiwango cha juu kuwahi kutolewa na Manispaa kwa vikundi vya wajasiriamali  "haya ni mafanikio makubwa sana kwa Manispaa  na wajasiliamali kwani dhana ya mikopo hii ni kukukuza uchumi.

Pamoja na kutoa fedha kwa vikundi lakini pia Manispaa imefanikiwa kutoa bajaji 45, pikipiki 22 na toyo 1 vikundi vya vijana na walemavu "tunaimani vyombo hivi vya usafiri vitaanza kuwaingizia kipato,  nawasii muanze marejesho haraka zaidi" alisisitiza Kebwe.

Akiongea kwa niaba  ya wajasiriamali wenzake  stuwart  Simon banda kutoka kikundi cha  jiwezeshe  Goba ameishukuru serikali na Manispaa  ya ubungo kwa kutoa mikopo kwa wajasiriamali  ili kukuza mitaji ya biashara  zetu zitakazotusaidia kujikwamua kiuchumi.

Taarifa

  • KIBALI CHA KUANZA KUTOZA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA MIZIGO July 17, 2023
  • KUKANUSHA TAARIFA YA UWEPO WA HARAFU MBAYA STENDI YA MABASI MAGUFULI July 06, 2023
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 Ubungo September 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KATA YA UBUNGO YAKABIDHI MKOPO WA TSH. 122,800,000/= KWA VIKUNDI SITA VYA ASILIMIA 10

    May 02, 2025
  • KAMPENI YA KATAA UCHAFU, SAFISHA, PENDESHA UBUNGO YAZINDULIWA, MITAA SAFI NA MICHAFU KUPEWA ZAWADI

    May 03, 2025
  • FANYENI KAZI, MSIJALI MASILAHI BINAFSI" ~ CHALAMILA

    May 01, 2025
  • HUDUMA YA KUJIFUNGUA KWA UPASUAJI YAANZA RASMI KITUO CHA AFYA GOBA,WANANCHI WAKARIBISHWA

    April 30, 2025
  • Tazama zote

Video

KIWANJA CHAKO KINA HATI? | UMEKUWA UKISUMBULIWA NA MIGOGORO YA ARDHI? | KARIBU KWENYE ARDHI CLINIC
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa