• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Industry,Trade and Investments
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Human Resources Management and administration
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Communit Development
    • Vitengo
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
      • Procument Management
      • Government Communication
      • Finance and Accounts
      • Sports, Culture and Arts
      • Waste Management and Sanitation
      • Natural Resources and Environment Conservation
    • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Other Laws
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
      • iCHF
      • Lishe
      • Social welfare
    • Elimu
      • Pre and Primary Education
      • Elimu Sekondari
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
      • Ten Percent Loans
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

UBORESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA KWA WAZEE YAPENDEZESHA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAZEE DUNIANI

Posted on: October 3rd, 2020


 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo imeadhimisha siku ya Wazee duniani iliyosindikizwa na kaulimbiu isemayo “familia na jamii ishiriki kuwatunza wazee” kwa kutoa huduma mbalimbali kwa wazee ikiwemo upimaji wa afya na matibabu pamoja na kutoa kadi za bima ya afya (iCHF) ikiwa ni moja ya mkakati wa serikali wa kuboresha huduma za afya kwa wazee.

Utoaji wa huduma hizo za afya umefanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia tarehe 1 hadi 2 oktoba, 2020 na kilele kufanyika tarehe 3 oktoba, 2020  katika viwanja vya mnazimmoja jijini Dar es salaam ambapo wazee walipata fursa ya kupimwa magonjwa kama macho, kisukari, shinikizo la damu , moyo  pamoja na kinywa na meno pamoja na kupewa ushauri nasaa wa masuala mbalimbali.

Akizungumza kwa niaba ya wazee wenzake kwenye maadhimisho  hayo, Bibi Hafsa Ismail Yasile wa kata ya Makurumila Wilaya ya Ubungo, ameeleza kuwa siku ya wazee duniani  imekuwa nzuri sana kwakwe kwani amepata fursa ya kupata vipimo vya maradhi mbalimbali ikiwemo sukari ,  moyo, shinikizo la damu na amegundulika kuwa na ugonjwa wa shinikizo la damu ambapo ameshauriwa kuanza matibabu mapema.

Bibi Hafsa amesema faida ya kushiriki maadhimisho hayo amepata huduma za afya bure  jambo ambalo kwa wazee ni zuri ukizingatia wazee wengi hawana uwezo wa kifedha kugharamia matibabu yao  wakati wote “kwa kufika kwenye maadhimisho ya siku ya wazee nimebahatika kupata bima ya afya ( iCHF) ambayo itanisaidia kupata matibabu bure mwaka mzima kwenye kituo chochote cha kutolea huduma za afya”

Aidha, Bibi hafsa amewasii wazee wenzake kujenga utamaduni wa kushiriki kwenye shughuli mbalimbali zinazowahusu wao ili waweze kujua mambo mbalimbali kwa ustawi wa maisha yao “ siku nyingine wanapopata wito wowote  wawajibike kuitika badala kukaidi na kubaki kuilalamikia serikali kuwa haiwajali”

Kwa upande wake Mzee Abuu Juma Segamba kutoka kata ya Manzese Wilaya ya Ubungo ameipongeza  Serikali kwa kuweka utaratibu wa upimaji na utoaji wa huduma za afya bure kwa wazee na ameomba utaratibu huu uwe endelevu.

Mzee Segamba amefafanua kuwa, miaka ya nyuma wazee walikuwa wakiachwa nyuma ila kuanzia mwaka 2018 mpaka mwaka huu wazee wamekumbukwa kwa kupewa  kipaumbele kwenye mambo mbalimbali ikiwemo kwenye huduma za afya.

Mmoja wa wazee wakipata akifanyiwa uchunguzi  kwenye maadhimisho ya siku wazee duniani iliyoadhimishwa kimkoa katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam leo tarehe 3 oktoba, 2020

Aidha Mzee Segamba ameeleza kuwa wazee hasa wanaume bado wameachwa nyuma kushirikishwa kwenye Nyanja ya utoaji maamuzi na utungaji wa sera ikiwemo kutokuwa na uwakilishi bungeni.

“Ukiangalia makundi kama ya wanawake, vijana na walemavu wamepewa kipaumbele katika bunge ambapo wanapata uwakilishi bungeni kupitia uwepo wa nafasi za viti maalumu lakini wazee hasa wanaume hatuna fursa hiyo, hivyo tunaiomba serikali itupatie fursa ya kupata uwakilishi vyombo vya maamuzi kuanzi kwenye mabaraza ya madiwani na bungeni kama yalivyo makundi ya wenzetu” ameomba  Mzee Segamba.

Aidha mwakilishi wa wazee jijini Dar es salaam ametumia siku hii ya wazee kutoa rai kwa serikali kuweka sheria itakayowafanya watoto kuwajibika kuwatunza wazee na wasipotekeleza wachukuliwe hatua za kisheria kama makosa mengine, kwa kufanya hivyo familia itakuwa imeshiriki kwa vitendo kuwatunza wazee kama kaulimbui ya maadhimisho haya  ya mwaka huu inavyosema “familia na jamii ishiriki kuwatunza wazee”

Tanzania inaungana na nchi nyingine za umoja wa mataifa kuadhimisha siku hii kwa mujibu wa Azimio la Umoja wa Mataifa Na. 49 ya Mwaka 1991 kila mwaka, lengo ikiwa kuhamasisha jamii kuweza kulinda na kutetea haki za wazee duniani kote pamoja na kutatua changamoto zinazowakabili na kuweka mipango ya kuzitatua ili waishi kwa heshima, hadhi na kuthaminiwa.

IMEANDALIWA NA;

Kitengo cha habari na uhususiano

Halmashauri ya manispaa ya ubungo

 

Taarifa

  • KIBALI CHA KUANZA KUTOZA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA MIZIGO July 17, 2023
  • KUKANUSHA TAARIFA YA UWEPO WA HARAFU MBAYA STENDI YA MABASI MAGUFULI July 06, 2023
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 Ubungo September 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KATA YA UBUNGO YAKABIDHI MKOPO WA TSH. 122,800,000/= KWA VIKUNDI SITA VYA ASILIMIA 10

    May 02, 2025
  • KAMPENI YA KATAA UCHAFU, SAFISHA, PENDESHA UBUNGO YAZINDULIWA, MITAA SAFI NA MICHAFU KUPEWA ZAWADI

    May 03, 2025
  • FANYENI KAZI, MSIJALI MASILAHI BINAFSI" ~ CHALAMILA

    May 01, 2025
  • HUDUMA YA KUJIFUNGUA KWA UPASUAJI YAANZA RASMI KITUO CHA AFYA GOBA,WANANCHI WAKARIBISHWA

    April 30, 2025
  • Tazama zote

Video

KIWANJA CHAKO KINA HATI? | UMEKUWA UKISUMBULIWA NA MIGOGORO YA ARDHI? | KARIBU KWENYE ARDHI CLINIC
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa