• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Industry,Trade and Investments
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Human Resources Management and administration
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Communit Development
    • Vitengo
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
      • Procument Management
      • Government Communication
      • Finance and Accounts
      • Sports, Culture and Arts
      • Waste Management and Sanitation
      • Natural Resources and Environment Conservation
    • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Other Laws
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
      • iCHF
      • Lishe
      • Social welfare
    • Elimu
      • Pre and Primary Education
      • Elimu Sekondari
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
      • Ten Percent Loans
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

WAMILIKI VITUO VYA KULELEA WATOTO (DAYCARE) WAPEWA MAFUNZO

Posted on: January 23rd, 2021

Wamiliki wa vituo vya watoto walio chini ya miaka mitano (DAYCARE) katika Manispaa ya Ubungo jijini Dar Es salaam, wamepatiwa mafunzo maalumu  yanayolenga kufahamu sheria, kanuni na taratibu na miongozo ya uendeshaji wa vituo hivyo ili kutoa huduma bora  ya malezi kwa watoto.

Mafunzo hayo yametolewa leo januari 23, 2021 na Manispaa ya Ubungo kupitia idara ya afya na ustawi wa jamii ambapo wamiliki 321 kati ya 600 wameshiriki mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi  wa Lapaz mtaa  wa Luguluni.

Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto  wadogo mchana maarufu kama Daycare wapatiwa mafunzo juu ya taratibu kanuni na sheria za kuendesha vituo hivyo.


Akitoa maelezo wakati wa kufungua mafunzo hayo Afisa ustawi  wa Manispaa ya Ubungo Zainabu Masilamba , alisema kuwa Manispaa kupitia kitengo cha ustawi wa jamii imeamua kuendesha mafunzo kwa wamiliki hao kutokana na ongezeko kubwa la uanzishwaji wa  vituo hivyo  vya kulelea watoto wadogo ambavyo havina usajili  jambo ambalo ni kinyume na taratibu.


Masilamba alieleza kuwa, kwa mujibu wa kanuni za mwaka 2014 sura ya 13 kupitia sheria ya mtoto namba 21 ya mwaka 2009 inaelekeza ili  kituo cha kulelea watoto wadogo mchana kiweze kufanya kazi lazima kuzingatia vigezo ambavyo vitamwezesha mtoto kuwa katika mazingira salama ya kujifunza elimu ya malezi ya  awali


Baada ya mafunzo haya ya kujenga uelewa, tunategemea wamiliki wa vituo ambavyo vinaendeshwa kinyume na taratibu, sheria na miongozo watatumia muda huu uliobaki kurekebisha kasoro zilizopo ili wasifungiwe vituo wakati wa zoezi la kufunga vituo visivyo na sifa mwishoni mwa mwezi machi.

Masilamba  anasema " tarehe 24 machi mwaka huu,  Manispaa ya Ubungo itafunga vituo vyote ambavyo vinaendesha huduma ya kulea watoto wadogo mchana kinyume na taratibu, kanuni miongozo na sheria ya kuendesha vituo hivyo ikwemo kutosajiliwa na kuto kidhi vigezo vya kutoa huduma ya  malezi ya awali kwa  watoto wadogo"

Aidha wamiliki wamekumbushwa kuzingatia ukubwa wa  eneo litakalo mwezesha mtoto  kujifunza kwa vitendo, uwepo wa miundombinu mizuri  hasa vyoo, usafi wa mazingira na pamoja na kuwa na  walezi waliopata mafunzo katika vyuo vya Montesol vinavyotambulika na serikali na kamishina wa ustawi wa jamii.

Wito umetolewa kwa wamiliki wa vituo vya kutoa huduma ya malezi ya awali kwa watoto wadogo mchana kutochanganya (daycare) na huduma zitolewazo katika shule za awali (nursery school) ikiwemo kuandika

Frank Andrea Kimaro ni kati ya wamiliki wa vituo waliopata mafunzo hayo, ameeleza kuwa mafunzo  hayo yamemuongezea uelewa zaidi wa namna ya kuendesha kituo chake lakini pia vitu au huduma anayostahili mtoto mdogo kutoka kwenye kituo.

Manispaa ya Ubungo ina jumla ya vituo 606  vinavyotoa huduma ya kulea watoto  wadogo mchana na kati hivyo ni vituo 100 vimesajiliwa 


Mganga mkuu wa Manispaa ya Ubungo Dkt Peter Nsanya akisisitiza jambo kwa wamiliki wa vituo wakati wa mafunzo. Amewakumbusha umuhimu wa kujiunga na bima ya afya ya jamii iliyoboreshwa (iCHF) ili kuwa na uhakika wa matibabu kwa gharama nafuu. 

Taarifa

  • KIBALI CHA KUANZA KUTOZA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA MIZIGO July 17, 2023
  • KUKANUSHA TAARIFA YA UWEPO WA HARAFU MBAYA STENDI YA MABASI MAGUFULI July 06, 2023
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 Ubungo September 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KATA YA UBUNGO YAKABIDHI MKOPO WA TSH. 122,800,000/= KWA VIKUNDI SITA VYA ASILIMIA 10

    May 02, 2025
  • KAMPENI YA KATAA UCHAFU, SAFISHA, PENDESHA UBUNGO YAZINDULIWA, MITAA SAFI NA MICHAFU KUPEWA ZAWADI

    May 03, 2025
  • FANYENI KAZI, MSIJALI MASILAHI BINAFSI" ~ CHALAMILA

    May 01, 2025
  • HUDUMA YA KUJIFUNGUA KWA UPASUAJI YAANZA RASMI KITUO CHA AFYA GOBA,WANANCHI WAKARIBISHWA

    April 30, 2025
  • Tazama zote

Video

KIWANJA CHAKO KINA HATI? | UMEKUWA UKISUMBULIWA NA MIGOGORO YA ARDHI? | KARIBU KWENYE ARDHI CLINIC
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa