• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Ubungo Municipal Council

  • Home
  • About US
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Secondary Education
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Industry,Trade and Investments
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Human Resources Management and administration
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Communit Development
    • Units
      • Legal Services
      • Internal Audit
      • ICT
      • Procument Management
      • Government Communication
      • Finance and Accounts
      • Sports, Culture and Arts
      • Waste Management and Sanitation
      • Natural Resources and Environment Conservation
    • Municipal By Laws
      • Municipal By Laws
      • Other Laws
  • Opportunities
    • Livestock
    • Agriculture
    • Markets
    • Bus Terminal
    • Industries
  • Services
    • Health
      • iCHF
      • Nutrition
      • Social welfare
    • Education
      • Pre and Primary Education
      • Secondary Education
    • Business
      • Service levy
      • Tax Registration
      • Business Licence
      • Hotel Levy
    • Enterpreneurship
      • Ten Percent Loans
    • Agriculture
    • Fishing
    • Livestock
      • UJUWA
  • Councilors
    • Councilors list
    • Council Committee
    • Council legal meeting
    • Meyor's schudule
  • Projects
    • Planned Projects
    • On going Projects
    • Completed projects
  • Publications
    • Guidelines
    • Application Forms
    • Reports
    • Acts
    • Bronchures
    • Tender Advert
    • Strategic Plan
    • Newsletter
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Press Release
    • Speeches

MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

Posted on: April 20th, 2023



Waziri Mkuu wa Jamhuri Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) azitaka Wizara ya TAMISEMI na wizara ya Ardhi kutenga maeneo ya Uwekezaji kwa ajili ya kuwezesha uwekezaji Nchini.

Sambamba na hilo amewataka Watanzania kuthamini uwekezaji mkubwa unaofanyika Ubungo na maeneo mengine na kuwaasa vijana wanaopata ajira kwenye miradi mbalimbali ya uwekezaji na amewataka wawekezaji kuzingatia Watanzania wote waliawajiri wanapata stahiki zao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za Nchi yetu.

Maelekezo hayo ameyatoa leo tarehe 20/04/2023 wakati anakagua mradi wa ujenzi wa kituo cha biashara cha kimataifa kinachojengwa katika manispaa ya ubungo eneo la stendi kuu ya zamani ya mabasi yaendayo mikoani.



Mhe. Majaliwa ameendelea kueleza kuwa kituo hicho kina maslahi makubwa kwa wananchi wa Ubungo na Taifa kwa ujumla kwani kitaenda kuchochea ongezeko la ajira, ukuaji wa uchumi kwani mapato ya Manispaa ya Ubungo yataongezeka na ametoa wito kwa wananchi wa Dar es Salaam kuchangamkia fursa ya uwepo wa kituo hicho cha kimataifa cha kibiashara.

“Serikali itaendelea kujenga mazingira mazuri ya kuvutia wawekezaji hapa nchini kutoka ndani na nje ya nchi na itaendelea kutangaza vivutio vya uwekezaji vilivyopo hapa nchini kwa maslahi mapana ya watanzania” alisema Mhe. Majaliwa

Akiongea Mhe. Anjella Kairuki Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI amesema mnamo tarehe 16/12/2023 Manispaa ya Ubungo iliingia mkataba na kampuni ya Shanghai Linghang group limited ambae ni mwekezaji aliyewekeza kwenye eneo la Ubungo ilipokuwa stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani kwa ajili ya kujenga kituo cha kimataifa cha kibiashara na mkataba huo kila baada ya miaka mitatu utafanyiwa marejeo na mapitio na kuboreshwa kwa mujibu wa bei za soko.

Mhe. Kairuki ameendelea kueleza kuwa uwekezaji huo unathamani ya dola 81,827,655.01 sawa na fedha za kitanzania shilingi bilioni 195 na mwekezaji atakuwa amerejesha fedha za uwekezaji baada ya muda wa uwekezaji kuisha na atatakiwa kukabidhi umiliki wa asilimia 100 kwa Manispaa ya Ubungo.

Aidha, Mhe. Kairuki amesema kituo hicho kitazalisha ajira rasmi za moja kwa moja zaidi ya 15,000 na zisizo za moja kwa moja zaidi ya 50,000 na kitakuwa na maduka ya ukubwa tofauti tofauti zaidi ya 2,000 na pia wafanyabiashara watapata fursa ya umiriki wa moja kwa moja wa maduka yao.


Kampuni ya Shanghai Linghang group limited imeiteua kampuni ya EAST AFRICA COMMERCIAL & LOGISTICS CENTER (EACLC) kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho, alieleza Mhe. Kairuki

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya EACLC Ndg. Catty Wang ameishikuru Serikali ya Tanzania kwa kuipa kibali cha ujenzi wa mradi huo na kusema mradi huo utakamilika mnamo mwezi Juni 2024 na mara moja biashara ziataanza kufanyika.

Catty amesema mradi huo utakuza biashara ndogo ndogo na kupanua biashara hizo ndani ya soko kubwa la Afrika kwani watanzania watapata fursa ya kuagiza na kuuza bidhaa nje ya Tanzania.

“Katika kuendesha uwekezaji wetu Nchini Tanzania kampuni ya EACLC limited itaendelea kutekeleza misingi ya ukweli, matokeo ya uhakika na imani njema kuhusu ushirikiano na Afrika ambao ni msingi uliowekwa na Mhe. Rais wa China Xi Jinping alipokuwa Dar es salaam miaka 10 iliyopita na pia Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuwa Nchini China hivi karibuni” aliahidi Wang.

Announcements

  • KIBALI CHA KUANZA KUTOZA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA MIZIGO July 17, 2023
  • KUKANUSHA TAARIFA YA UWEPO WA HARAFU MBAYA STENDI YA MABASI MAGUFULI July 06, 2023
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 Ubungo September 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • View All

Latest News

  • MIRADI 7 YENYE THAMANI YA BILIONI 8.2 UBUNGO YAPITA KWA KISHINDO MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025

    June 05, 2025
  • TUZINGATIE USAFI KUEPUKA MAGONJWA

    May 31, 2025
  • BODI YA AFYA UBUNGO YAPONGEZA WATAALAM WA AFYA NA KUTOA MAAGIZO YAKUBORESHA NYANJA MBALIMBALI

    May 29, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNATANGAZA UTEKELEZAJI WA MIRADI KWA WANANCHI

    May 24, 2025
  • View All

Video

KIWANJA CHAKO KINA HATI? | UMEKUWA UKISUMBULIWA NA MIGOGORO YA ARDHI? | KARIBU KWENYE ARDHI CLINIC
More Videos

Quick Links

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Related Links

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Postal Address: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Mobile:

    Email: md@ubungomc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Site Map

Copyright ©2017Ubungo Municipal Council All rights reserved.