- Mwanzo
- Kuhusu sisi
-
Utawala
- Muundo
-
Idara
- Elimu Sekondari
- Agriculture, Livestock and Fisheries
- Industry,Trade and Investments
- Planning and Coordination
- Infrastructure, Rural and Urban Development
- Pre-Primary and Primary Education
- Human Resources Management and administration
- Health, Social Welfare and Nutrition Services
- Communit Development
- Vitengo
- Sheria ndogo ndogo za Manispaa
- Fursa za Uwekezaji
- Huduma zetu
- Madiwani
- Miradi
- Machapisho
- Kituo cha Habari
Akiongea Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Manispaa ya Ubungo Dkt Peter Nsanya amewaeleza wageni hao namna Manispaa hiyo inasimamia ukusanyaji wa mapato kwa ufanisi ambapo kila kata inamlezi wake ambao ni wakuu wa idara na Vitengo na maafisa biashara ambao wamekuwa wakishirikiana na viongozi wa Kata wanazozilea katika kuhakikisha mapato yanakusanywa kwa usahihi na ufanisi
Nsanya ameendelea kueleza kuwa uwepo wa Kituo cha Magufuli umekuwa ni chachu ya kuongeza mapato kwa Manispaa hiyo ambapo kwa mwaka kituo hicho kinakusanya shilingi Bilioni 5 kutoka kwenye vyanzo vyake ikiwemo ushuru wa kuingilia kituoni, vyooni, bajaji na pikipiki, hoteli inayosimamiwa na mzabuni, parking za kulaza magari, Ada ya kuingiza na kutoa mabasi kituoni na upangishaji wa fremu za biashara.
Nae Mhe. Kheri James Mkuu wa Wilaya ya Ubungo amesema Mkoa wa Dar es Salaam ambao Wilaya ya Ubungo ipo ndani yake na Mkoa wa Mwanza inakimbizana katika wingi wa watu hivyo ni lazima kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake na hivyo ni vyema kubadilishana uzoefu kwa mazuri yanayofanywa na Halmashauri za mikoa hiyo.

