• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Industry,Trade and Investments
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Human Resources Management and administration
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Communit Development
    • Vitengo
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
      • Procument Management
      • Government Communication
      • Finance and Accounts
      • Sports, Culture and Arts
      • Waste Management and Sanitation
      • Natural Resources and Environment Conservation
    • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Other Laws
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
      • iCHF
      • Lishe
      • Social welfare
    • Elimu
      • Pre and Primary Education
      • Elimu Sekondari
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
      • Ten Percent Loans
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

Posted on: April 20th, 2023



Waziri Mkuu wa Jamhuri Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) azitaka Wizara ya TAMISEMI na wizara ya Ardhi kutenga maeneo ya Uwekezaji kwa ajili ya kuwezesha uwekezaji Nchini.

Sambamba na hilo amewataka Watanzania kuthamini uwekezaji mkubwa unaofanyika Ubungo na maeneo mengine na kuwaasa vijana wanaopata ajira kwenye miradi mbalimbali ya uwekezaji na amewataka wawekezaji kuzingatia Watanzania wote waliawajiri wanapata stahiki zao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za Nchi yetu.

Maelekezo hayo ameyatoa leo tarehe 20/04/2023 wakati anakagua mradi wa ujenzi wa kituo cha biashara cha kimataifa kinachojengwa katika manispaa ya ubungo eneo la stendi kuu ya zamani ya mabasi yaendayo mikoani.



Mhe. Majaliwa ameendelea kueleza kuwa kituo hicho kina maslahi makubwa kwa wananchi wa Ubungo na Taifa kwa ujumla kwani kitaenda kuchochea ongezeko la ajira, ukuaji wa uchumi kwani mapato ya Manispaa ya Ubungo yataongezeka na ametoa wito kwa wananchi wa Dar es Salaam kuchangamkia fursa ya uwepo wa kituo hicho cha kimataifa cha kibiashara.

“Serikali itaendelea kujenga mazingira mazuri ya kuvutia wawekezaji hapa nchini kutoka ndani na nje ya nchi na itaendelea kutangaza vivutio vya uwekezaji vilivyopo hapa nchini kwa maslahi mapana ya watanzania” alisema Mhe. Majaliwa

Akiongea Mhe. Anjella Kairuki Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI amesema mnamo tarehe 16/12/2023 Manispaa ya Ubungo iliingia mkataba na kampuni ya Shanghai Linghang group limited ambae ni mwekezaji aliyewekeza kwenye eneo la Ubungo ilipokuwa stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani kwa ajili ya kujenga kituo cha kimataifa cha kibiashara na mkataba huo kila baada ya miaka mitatu utafanyiwa marejeo na mapitio na kuboreshwa kwa mujibu wa bei za soko.

Mhe. Kairuki ameendelea kueleza kuwa uwekezaji huo unathamani ya dola 81,827,655.01 sawa na fedha za kitanzania shilingi bilioni 195 na mwekezaji atakuwa amerejesha fedha za uwekezaji baada ya muda wa uwekezaji kuisha na atatakiwa kukabidhi umiliki wa asilimia 100 kwa Manispaa ya Ubungo.

Aidha, Mhe. Kairuki amesema kituo hicho kitazalisha ajira rasmi za moja kwa moja zaidi ya 15,000 na zisizo za moja kwa moja zaidi ya 50,000 na kitakuwa na maduka ya ukubwa tofauti tofauti zaidi ya 2,000 na pia wafanyabiashara watapata fursa ya umiriki wa moja kwa moja wa maduka yao.


Kampuni ya Shanghai Linghang group limited imeiteua kampuni ya EAST AFRICA COMMERCIAL & LOGISTICS CENTER (EACLC) kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho, alieleza Mhe. Kairuki

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya EACLC Ndg. Catty Wang ameishikuru Serikali ya Tanzania kwa kuipa kibali cha ujenzi wa mradi huo na kusema mradi huo utakamilika mnamo mwezi Juni 2024 na mara moja biashara ziataanza kufanyika.

Catty amesema mradi huo utakuza biashara ndogo ndogo na kupanua biashara hizo ndani ya soko kubwa la Afrika kwani watanzania watapata fursa ya kuagiza na kuuza bidhaa nje ya Tanzania.

“Katika kuendesha uwekezaji wetu Nchini Tanzania kampuni ya EACLC limited itaendelea kutekeleza misingi ya ukweli, matokeo ya uhakika na imani njema kuhusu ushirikiano na Afrika ambao ni msingi uliowekwa na Mhe. Rais wa China Xi Jinping alipokuwa Dar es salaam miaka 10 iliyopita na pia Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuwa Nchini China hivi karibuni” aliahidi Wang.

Taarifa

  • KIBALI CHA KUANZA KUTOZA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA MIZIGO July 17, 2023
  • KUKANUSHA TAARIFA YA UWEPO WA HARAFU MBAYA STENDI YA MABASI MAGUFULI July 06, 2023
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 Ubungo September 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KATA YA UBUNGO YAKABIDHI MKOPO WA TSH. 122,800,000/= KWA VIKUNDI SITA VYA ASILIMIA 10

    May 02, 2025
  • KAMPENI YA KATAA UCHAFU, SAFISHA, PENDESHA UBUNGO YAZINDULIWA, MITAA SAFI NA MICHAFU KUPEWA ZAWADI

    May 03, 2025
  • FANYENI KAZI, MSIJALI MASILAHI BINAFSI" ~ CHALAMILA

    May 01, 2025
  • HUDUMA YA KUJIFUNGUA KWA UPASUAJI YAANZA RASMI KITUO CHA AFYA GOBA,WANANCHI WAKARIBISHWA

    April 30, 2025
  • Tazama zote

Video

KIWANJA CHAKO KINA HATI? | UMEKUWA UKISUMBULIWA NA MIGOGORO YA ARDHI? | KARIBU KWENYE ARDHI CLINIC
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa