• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Industry,Trade and Investments
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Human Resources Management and administration
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Communit Development
    • Vitengo
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
      • Procument Management
      • Government Communication
      • Finance and Accounts
      • Sports, Culture and Arts
      • Waste Management and Sanitation
      • Natural Resources and Environment Conservation
    • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Other Laws
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
      • iCHF
      • Lishe
      • Social welfare
    • Elimu
      • Pre and Primary Education
      • Elimu Sekondari
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
      • Ten Percent Loans
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

MASHINDANO YA UMISETA MANISPAA YA UBUNGO YAFUNGWA LEO.

Posted on: June 17th, 2022

Mashindano ya UMISETA wilaya ya Ubungo yaliyokua yakifanya katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola iliyopo Mabibo, yamefungwa rasmi leo kwa timu ya kanda ya Ubungo kuibuka mabingwa.

Mashindano hayo yalikua yakishirikisha timu za shule mbalimbali za Wilaya ya Ubungo ambapo zilichujwa na kupatikana timu tatu za kanda tatu ambazo ni kanda ya Kibamba, Kanda ya Goba na kanda ya Ubungo ambapo baada ya hatua mbalimbali za mashindano hayo leo Juni 17 ilikua ni fainali kati ya kanda ya Kibamba dhidi ya kanda ya Ubungo.

Mashindano hayo yalikua ni maalumu ili kuchagua wanafunzi watakaounda timu ya Manispaa ya Ubungo ambayo itaenda kushiriki mashindano ya mkoa yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Julai 26 mpaka Julai 30, 2022.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi, Afisa elimu sekondari Manispaa ya Ubungo ndugu Voster Mgina amesema kuwa mashindano hayo yamefanyika kwa mafanikio makubwa kwa sababu wilaya ya Ubungo ina vijana wenye vipaji vikubwa katika michezo mbalimbali na kuwa timu ya Wilaya iliyopatikana ni nzuri na matumaini ni kuwa itaenda kufanya vizuri kwenye mashindano ya mkoa
Naye mgeni rasmi wa mashindano hayo meneja wa benki ya NMB tawi la chuo kikuu cha Dar es salaam, ndugu Msafiri Hamza Mfinanga amesema kuwa mashindano ya michezo kwa wanafunzi mashuleni ni jambo muhimu sana kwa afya ya mwili na akili kwa wanafunzi hao na wao kama benki wataendelea kushirikiana na serikali kwenye programu mbalimbali za michezo kwa wilaya ya Ubungo.

"Benki ya NMB ipo karibu na watu wa makundi mbalimbali wakiwemo wanafunzi hivo basi wataendelea kuwa karibu na jamii kwa kutoa misaada mbalimbali ikiwemo misaada ya vifaa vya michezo kwa wanafunzi" alisema.

Aidha, Afisa utamaduni Manispaa ya Ubungo ndugu Kassim Semfuko amewapongeza wakuu wa shule mbalimbali za Manispaa ya Ubungo kwa usimamizi mzuri wa mashindano hayo kuanzia mwanzo mpaka mwisho na pia amewapongeza wanamichezo wanafunzi walioshiriki kwenye mashindano hayo na pia amewasihi kuendelea kulinda vipaji vyao ili siku moja vije kuwa ajira kwao na pia kuleta mchango mkubwa kwa taifa letu.



#UbungoYetuFahariYetu

Taarifa

  • KIBALI CHA KUANZA KUTOZA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA MIZIGO July 17, 2023
  • KUKANUSHA TAARIFA YA UWEPO WA HARAFU MBAYA STENDI YA MABASI MAGUFULI July 06, 2023
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 Ubungo September 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KATA YA UBUNGO YAKABIDHI MKOPO WA TSH. 122,800,000/= KWA VIKUNDI SITA VYA ASILIMIA 10

    May 02, 2025
  • KAMPENI YA KATAA UCHAFU, SAFISHA, PENDESHA UBUNGO YAZINDULIWA, MITAA SAFI NA MICHAFU KUPEWA ZAWADI

    May 03, 2025
  • FANYENI KAZI, MSIJALI MASILAHI BINAFSI" ~ CHALAMILA

    May 01, 2025
  • HUDUMA YA KUJIFUNGUA KWA UPASUAJI YAANZA RASMI KITUO CHA AFYA GOBA,WANANCHI WAKARIBISHWA

    April 30, 2025
  • Tazama zote

Video

KIWANJA CHAKO KINA HATI? | UMEKUWA UKISUMBULIWA NA MIGOGORO YA ARDHI? | KARIBU KWENYE ARDHI CLINIC
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa