• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Industry,Trade and Investments
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Human Resources Management and administration
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Communit Development
    • Vitengo
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
      • Procument Management
      • Government Communication
      • Finance and Accounts
      • Sports, Culture and Arts
      • Waste Management and Sanitation
      • Natural Resources and Environment Conservation
    • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Other Laws
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
      • iCHF
      • Lishe
      • Social welfare
    • Elimu
      • Pre and Primary Education
      • Elimu Sekondari
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
      • Ten Percent Loans
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

MIKOPO YA HALMASHAURI YACHOCHEA MAFANIKIO YA WAJASIRIAMALI

Posted on: September 30th, 2025

Mpango wa utoaji wa mikopo midogo ya asilimia 10 inayotokana na makusanyo ya mapato ya ndani kwa vikundi vya wajasiriamali katika Manispaa ya Ubungo umeendelea kuleta mafanikio makubwa ya kijamii na kiuchumi, kwa kuwawezesha wanufaika kuanzisha na kukuza biashara zao, kujiajiri, na kuongeza kipato.

Mikopo hiyo, iliyotolewa kati ya Januari na Machi 2025 imewezesha vikundi mbalimbali kuanzisha na kupanua biashara ndogo, jambo ambalo limewasaidia kujiajiri na kuboresha hali zao za maisha.

Mojawapo ya mafanikio hayo yanatokana na kikundi cha Ukurasa Mpya kilichopo Kata ya Makuburi, ambacho kinajihusisha na uzalishaji wa siagi ya karanga. Mwenyekiti wa kikundi hicho, Bi. Blandina Samuel Pima, amesema mkopo walioupata umeleta mabadiliko makubwa katika shughuli zao za kiuchumi.

"Hapo awali tulikuwa tukizalisha majumbani mwetu kwa vifaa duni. Sasa tumepata eneo rasmi la uzalishaji, tumenunua mashine za kisasa pamoja na malighafi muhimu. Kweli mkopo umetuwezesha kupiga hatua kubwa," alisema Bi. Pima akiwa katika ofisi yao mpya ya uzalishaji.

Kadhalika, kikundi cha NEH Women Group, kinachojishughulisha na usambazaji wa vyakula katika maeneo mbalimbali, kimenufaika kwa kiasi kikubwa na mkopo huo. Bi. Fatuma Issa Faru, Mhazini wa kikundi hicho, alieleza kuwa mkopo huo umeimarisha biashara yao kwa kiasi kikubwa.

"Tunaishukuru serikali kwa kutupatia mkopo huu ambao ni mkombozi mkubwa kwa biashara yetu. Tumejipanga kuhakikisha tunarejesha kwa wakati kama njia ya kuendeleza mpango huu kwa wengine," alibainisha.

Vikundi vingine vilivyonufaika na mpango huo ni pamoja na Car Body Work and Painting, Nyota Njema Group, na Genius Group, vyote kutoka Kata ya Sinza. Pia, kunavikundi vingine kutoka Kata za Kimara, Ubungo, na Saranga ambavyo vimepata manufaa kama hayo.

Afisa Maendeleo ya Jamii wa Kata ya Kimara, Bi. Ketra Mwakimi, ametoa wito kwa vikundi zaidi kujitokeza kuchukua mikopo hii kwa lengo la kujikwamua kiuchumi na kuchangia ajenda ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kupunguza ukosefu wa ajira kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Taarifa

  • KIBALI CHA KUANZA KUTOZA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA MIZIGO July 17, 2023
  • KUKANUSHA TAARIFA YA UWEPO WA HARAFU MBAYA STENDI YA MABASI MAGUFULI July 06, 2023
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 Ubungo September 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MIKOPO YA HALMASHAURI YACHOCHEA MAFANIKIO YA WAJASIRIAMALI

    September 30, 2025
  • UBUNGO YAAHIDI KUJIPANGA IMARA ZAIDI KWA MSIMU UJAO WA SHIMISEMITA | YAPOTEZA MBELE YA DODOMA JIJI

    August 29, 2025
  • WANANCHI MSIGANI WAANZA KUNUFAIKA NA MAFUNZO YA KILIMO MJINI.

    August 29, 2025
  • MAAFISA UBUNGO WATOA CHANJO KWA NG"OMBE YA HOMA YA MAPAFU

    August 22, 2025
  • Tazama zote

Video

KIWANJA CHAKO KINA HATI? | UMEKUWA UKISUMBULIWA NA MIGOGORO YA ARDHI? | KARIBU KWENYE ARDHI CLINIC
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa