• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Industry,Trade and Investments
      • Planning and Coordination
      • Infrastructure, Rural and Urban Development
      • Pre-Primary and Primary Education
      • Human Resources Management and administration
      • Health, Social Welfare and Nutrition Services
      • Communit Development
    • Vitengo
      • Legal Services
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
      • Procument Management
      • Government Communication
      • Finance and Accounts
      • Sports, Culture and Arts
      • Waste Management and Sanitation
      • Natural Resources and Environment Conservation
    • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Sheria ndogo ndogo za Manispaa
      • Other Laws
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
      • iCHF
      • Lishe
      • Social welfare
    • Elimu
      • Pre and Primary Education
      • Elimu Sekondari
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
      • Ten Percent Loans
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

WATENDAJI KATA UBUNGO WASAINISHWA MIKATABA YA LISHE

Posted on: October 31st, 2022


Manispaa ya Ubungo kupitia Idara ya Afya kitengo cha Lishe imewapa mikataba watendaji wa Kata za Manispaa hiyo lengo ikiwa ni kuendelea kusimamia mikakati ya Serikali juu ya suala la lishe bora kwa raia wake.

Usainishwaji huo umefanyika Leo tarehe 31 Oktoba, 2022 ambapo Watendaji Kata hao wamesaini mikataba hiyo yao na Manispaa hiyo na kutakiwa kwenda kuifanyia kazi kama mikataba hiyo inavyojieleza.

Akiongea Bi. Beatrice Mossile Afisa lishe wa Manispaa hiyo wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa lishe kwa ngazi ya Halmashauri kwa robo ya kwanza 2022/2023 amesema  Kitengo cha lishe  kimefanikiwa kutoa elimu kwa Madiwani 19, walimu wakuu wa Shule za msingi na Sekondari, walimu wa day care na walimu wa afya na kutibu utapiamlo.

Na hivyo kupelekea kuwepo kwa Shule 192 zenye club za afya na lishe Sawa na 74.4% kati ya Shule 258, Shule 90 za msingi na Sekondari zinazotumia unga wa mahindi uliowekwa virutubisho na kuwepo kwa mashine 7 za kusaga lishe sawa na 70% kati ya 10 zinazohitajika.

Mossile ameendelea kueleza kuwa Manispaa hiyo kwa sasa imefanikiwa kupambana na tatizo la udumavu kutoka 8% hadi kufikia 1.1% na hivyo matarajio ya Manispaa kwa sasa ni kuhakikisha idara ya elimu msingi na sekondari wanashirikiana vizuri na Kamati za shule, wazazi au walezi ili kukubaliana namna ya kuwezesha wanafunzi kupata chakula mashuleni kama muongozo wa lishe unavyoeleza.

Kwa upande wake Mhe. Kheri James Mkuu wa Wilaya ya Ubungo amesema ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha mpango wa lishe unasimamiwa vizuri na ametoa pongezi kwa Manispaa kwa kufanikiwa kupanbana na udumavu kutoka 8% hadi kufikia 1.1% na amezipongeza kata zilizofanya vizuri na ametoa wito kwa Kata zingine kuiga mfano wa Kata hizo.

James amewataka watendaji hao kuhakikisha wanafanya vikao na watendaji wa mitaa na walimu wakuu wa shule za kwenye maeneo yao, Kamati za shule, wazazi au walezi ili kujua namna bora ya kuwezesha watoto kupata chakula mashuleni.

Taarifa

  • KIBALI CHA KUANZA KUTOZA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA MIZIGO July 17, 2023
  • KUKANUSHA TAARIFA YA UWEPO WA HARAFU MBAYA STENDI YA MABASI MAGUFULI July 06, 2023
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 Ubungo September 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KATA YA UBUNGO YAKABIDHI MKOPO WA TSH. 122,800,000/= KWA VIKUNDI SITA VYA ASILIMIA 10

    May 02, 2025
  • KAMPENI YA KATAA UCHAFU, SAFISHA, PENDESHA UBUNGO YAZINDULIWA, MITAA SAFI NA MICHAFU KUPEWA ZAWADI

    May 03, 2025
  • FANYENI KAZI, MSIJALI MASILAHI BINAFSI" ~ CHALAMILA

    May 01, 2025
  • HUDUMA YA KUJIFUNGUA KWA UPASUAJI YAANZA RASMI KITUO CHA AFYA GOBA,WANANCHI WAKARIBISHWA

    April 30, 2025
  • Tazama zote

Video

KIWANJA CHAKO KINA HATI? | UMEKUWA UKISUMBULIWA NA MIGOGORO YA ARDHI? | KARIBU KWENYE ARDHI CLINIC
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa